Alitoa pebdekezo hilo katika Twitter yake na kuongeza kuwa atawasilisha wazo hilo katika kikao cha baraza la mawaziri
Pia liweka picha inayoonesha mmea huo unavyokuwa:
On this one, the majority says: LEGALIZE IT!! I will put the proposal to legalize it at the Cabinet Lekgotla this January. The People have demanded it. But those medical doctors🙈🙈. 😳😳
— Tito Mboweni (@tito_mboweni)
Uuzaji wa bangi ya kiasi chochote ni kinyume cha sheria, kwa mujibu wa sheria za Afrika Kusini.
Je unazifahamu nchi zinazotumia bangi kwa kiasi kikubwa?
Lesotho
Matumizi ya bangi nchini Lesotho yanaruhusiwa tu kwa matumizi ya dawa, kwa kiasi kikubwa bangi hulimwa nchini humo. Miaka ya 2000 ilikadiriwa kuwa asilimia 70 ya bangi nchini Afrika Kusini inatoka nchini Lesotho.
Wakulima nchini Lesotho wanalima bangi kwa ajili ya matumizi yao nyumbani na kusafirisha nje ya mipaka, kutokana na hali ya umasikini waliyonayo, wakulima wadogo nchini humo wanalima bangi miongoni mwa mazao yao mengine kama vile mahindi kwa ajili ya kusafirisha nchini Afrika Kusini.
Zimbabwe kuhalalisha upanzi na matumizi ya bangi.
Korea Kaskazini
Bangi hukua kwa wingi sana nchini Korea Kaskazini hata mashirika ya kiserikali yamekuwa yakisafirisha kuuza nje ili kupata fedha za kigeni.
wachambuzi wa mambo wanasema haiko wazi kama kuna sheria inayopinga matumizi ya bangi, nchi hiyo haitazami kama matumizi ya bangi ni kinyume cha sheria.
Bangi imekuwa ikiuzwa kwenye maduka ya vyakula na hata maeneo mengine watu wakivuta bila kificho.