Lets Party! Corona Imeisha - Paul Makonda asema

PAUL-MAKONDA-730x414
PAUL-MAKONDA-730x414
Kamishna mkuu wa mji wa Dar El Salaam ameshtua ulimwengu baada ya kuwarai Watanzania kujitokeza kuanza kusherehekea  na hata kuingia mikahawani kwa kile amesema kuwa virusi hivyo havipo ,vimeisha.,

Paul Makonda  ,mkuu wa mji huo amesema hata maduka ya jumla ambayo asilimia 80 ya bidhaa zao zilikuwa zimeisha waakikisha kukuwa wanajaza bidhaa nyingine nyingi ili kuwapa watanzania fursa ya kujivinjari kabisa.

Taarifa za hivi maajuzi kutoka kwenye Ubalozi wa Amerika katika taifa hilo zilisema kuwa mji wa huo wa Dars El Salaam umejaa wagonjwa wa virusi hivyo hatari na hivyo itakuwa vigumu kwa taifa hilo kukimu idadi hiyo ya wagonjwa .

Ni zaidi ya mwezi mmoja sasa tangu taifa la Tanzania kutoa takwimu za watu walioathirikka na viryusi hivyo ,mswala ambalo linatia hofu kwa wakaazi wengi Tanzania.

Rais Magufuli alitupilia mbali wazo hilo la Amerika na kuwataka Watanzania wote kutenga siku tatu za maombi ili kuliombea taifa .

Siku chache zilizopita ,Magufulia aliamrisha kurejelewa kwa shughuli zote nchini humu ikiwemo michezo,Vyuo kufunguliwa na hata shughuli za Utalii kurejelea hali yake ya kawaida.

Sasa wakaazi wendi wa Dar Es Salaam wanahofia kuhusiana na tangazo hilo la Makonda wengi wakihofu kuwa huenda wataambukizwa virusi hivyo wakifuatwa himizo hilo.

Kufikia sasa Tanzania imesajili visa 509 vya maambukizi huku watu 21 wakiwa wamepoteza maisha kutokana na virusi hivyo.

.