Ligi ya Europa: Makali ya Pepe yaokolea Arsenal

pepe
pepe
Nicolas Pepe aliokolea Arsenal kwa free-kicks mbili katika dakika kumi za mwisho za mechi yao ya makundi ya ligi ya Uropa dhidi ya Vitoria Guimaraes waliposhinda mabao 3-2 ugani Emirates.

Walikua wanapoteza 2-1 wakati Pepe alipofunga bao kunako dakika ya 75th na lingine dakika tano baadae. Kwingineko Manchester United walipata ushindi wa 1-0 dhidi ya Red Star Belgrade.

Hayo yakijiri, wachezaji wa ligi ya Premier huenda wakabiliwa na uwezekano wa kucheza mechi siku sita kabla ya kuanza kwa olimpiki ya majira ya baridi mwaka 2020 huko Qatar.

https://radiojambo.co.ke/nameless-ampasha-massawe-baada-ya-kuanguka-katika-jangwa-la-dubai/

Mipango ya awali inaonyesha ratiba ya ligi hio kupangwa wakati wa mashindano hayo yatakayoanza Novemba tarehe 21 hadi Disemba tarehe 18. Mechi za ligi huenda zikachezwa kuanzia Novemba tarehe 12 na kuregelewa tarehe 26 Disemba, siku nane baada ya fainali. Suala hili litajadiliwa katika mkutano ujao wa wadau wa ligi hio mwezi ujao.

Polisi wa Merseyside wamewasaidia Liverpool kumtambua mhuhusika aliyechapisha bango la Divock Origi lililotajwa kuwa la kukera na la kibaguzi. Polisi wa Ubelgiji sasa wanasema wanachunguza kisa hicho ambapo picha ya Origi ilichapishwa mwishoni mwa mechi ya ligi ya mabingwa waliyowanyuka Genk jumatano, huku Uefa ikisubiri ripoti kutoka kwa shirika la kukabiliana ubaguzi wa rangi FARE.

https://radiojambo.co.ke/mwandishi-afungwa-kwa-kushiriki-ngono-nje-ya-ndoa/

Huenda Harambee Stars wakakabiliwa na sintofahamu katika siku chache zijazo wanapojitayarisha kwa michuano ya AFCON mwaka 2021 kwa kua FIFA imetishia kupiga marufuku FKF baada ya George Mwaura kuwasilisha kesi katika mahakama kuu kuahirisha uchaguzi unaokuja. Kanuni za FIFA zinaashiria kuwa masuala ya soka hayapaswi kushughulikiwa na mahakama za kawaida bali mahakama za spoti. Iwapo Mwaura hataondoa kesi hio anajiweka katika hatari ya kupigwa marufuku ya shughuli zote za soka.

Ligi ya Kenya cup inaanza kesho katika maeneo kadha. Mabingwa watetezi  KCB wataanza kampeni yao na mechi dhidi ya Western Bulls. Huko Nakuru katika uwanja wa maonyesho ya kilimo, Menengai Oilers watakabana na majirani zao Nakuru RFC huku Homeboyz wakichuana na Kenya Harlequins. Mechi zingine zitakua kati ya Kabras watakaowaalika Kisumu RFC, Mwamba watachuana na Blak Blad huku Impala wakikabana na Nondies katika uwanja wa Jamhuri.