Ligi ya Uingereza: ushindani wa kumaliza katika nne bora

Ligi ya Uingereza itakuwa inachezwa wikendi hii huku klabu mbali mbali zikiwa na matarajio ya kumaliza katika orodha ya nne bora katika msimu huu wa mwaka 2019/2020.

Vijana wake Pep Guardiola waliweza kumaliza kileleni katika msimu uliopita baada ya ushindani mkali kushuhudiwa kati yao na Liverpool.

 Kwa sasa  klabu ya Liverpool inaongoza kwenye ligi hiyo ikiwa na pointi 31, wakifuatiwa na Manchester City ambayo wameweza kupata pointi 25, huku Leicester na Chelsea wakifunga orodha ya nne bora kila mmoja akiandikisha pointi 23.

Michuano ambayo itachezwa wikendi hii itachangia pakubwa kuthibitisha klabu ambazo huenda ikamaliza katika nafasi ya nne bora msimu huu.

 Manchester United, Tottenham, na Arsenal pia ni miongoni mwa klabu ambazo zinatarajiwa kuleta ushindani mkubwa.

Mechi kubwa wikendi hii itakuwa baina ya Liverpool na Mancity ambao wanashikilia nafasi ya kwanza na pili mtawalia.

Mechi zingine ni;

Chelsea vs Crystal Palace

Tottenham vs Sheffield Utd

Leicester vs Arsenal

Man United vs Brighton