Liverpool ilichukua usukani wakati Joel Matip alipowaweka kifua mbele kwa bao thabiti la kichwa kutoka kwa kona iliyovurumishwa na Trent Alexander-Arnold dakika nne kabla ya mapumziko . Matumaini aliokuwa nayo kocha Unai Emery kuwatazama vijana wake wakijirejesha kwenye mchezo yalidimdimia wakati mchezaji mpya David Luiz alipomwelekeza Mohamed Salah katika safu ya nyuma katika dakika ya 49.
Mshambuliaji huyo raia wa Misri alifunga penalti na kisha kumfedhesha Luiz tena kwa pasi wa chini iliyotingisha nyavu kwa upande wa pembeni . Nguvu mpya wa arsenal Lucas Torreira aliifungua the gunners bao moja lakini hakuna ambacho kingeizuia Liverpool kusajili ushindi wao wa 12 mfululizo katika ligi ya premier na kusawazisha msururu wao bora chini ya Kenny Dalglish kati ya Aprili na Oktoa mwaka wa 1990.