Gwiji wa Liverpool Mohammed Salah aivuruga Arsenal kwa kufunga Mawili

Liverpool celebrating
Liverpool celebrating
Liverpool   iliendeleza uthabiti wao katika mwanzo wa ligi ya premier kwa  kuishinda arsenal mabaoa matatu kwa moja kwenye kabiliano la kufana uwanjani Anfield .The Gunners,   kilabu pekee kubwa katika ligi kushinda mechi zao mbili za mwanzo  walikuwa na fursa za kuilemea Liverpool   katika kipindi cha kwanza  hasa wakati mchezaji mpya aliyesainiwa kwa  pauni milioni 71 Nicolas Pepep alipomkabidhi mikononi mwakju mlinda lango  Adrian .

Liverpool  ilichukua usukani wakati Joel Matip alipowaweka kifua mbele  kwa bao thabiti la kichwa  kutoka kwa kona iliyovurumishwa na  Trent Alexander-Arnold dakika nne kabla ya mapumziko . Matumaini  aliokuwa nayo kocha Unai  Emery kuwatazama vijana wake wakijirejesha kwenye mchezo yalidimdimia wakati  mchezaji mpya David Luiz  alipomwelekeza  Mohamed Salah katika safu ya  nyuma katika dakika ya 49.

Mshambuliaji huyo raia wa Misri  alifunga penalti  na kisha kumfedhesha Luiz tena  kwa pasi  wa chini iliyotingisha nyavu  kwa upande wa pembeni .  Nguvu mpya wa arsenal  Lucas Torreira  aliifungua the gunners bao moja  lakini hakuna ambacho kingeizuia Liverpool kusajili ushindi wao wa 12 mfululizo katika ligi ya premier  na kusawazisha msururu wao bora  chini ya   Kenny Dalglish kati ya  Aprili na Oktoa mwaka wa  1990.