Maandamano yamezuka huko Kisii kabla ya ziara ya Naibu wa rais hivi leo .Maandamano ya yamefanywa na makundi yanayounga mkono mchakato wa BBI lakini wafuasi wa DP Ruto pia wamejitokeza kuyajibu kwa kufanyaa maandamano yao .
Ruto anatarajiwa kuzuri eneo la Kisii anapoendelea kuimarisha uungwaji mkono kutoka kwa wakaazi wa kaunti hiyo kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2022 .
Ziara yake hiyo inajiri siku mbili baada ya Ruto kuanda mkutano na viongozi walioachaguliwa kutoka eneo hilo katika makaazi yake rasmi mtaani Karen siku ya jumatatu .
Ruto anatarajiwa kupokelewa na viongozi wanaoendeleza kampeini zake katika eneo la Kisii naibu wa gavana wa kaunti hiyo Joash Maangi na mbunge wa mugirango kusini Sylvanus Osoro .
Duru zaarifu kwamba Ruto anatarajiwa kufanya mkutano mwingine na viongozi wa jamii ya Gusii baadaye mwezi ujao