Macho Man :Putin Huenda akazidisha muda wake kama Kiongozi wa Urusi .

 Rais  wa Urusi Vladimir Putin huenda ameanza kuchukua hatua za kuhakikisha kwamba anasalia madarakani hata baada ya kipindi chake kuhudumu kutamatika mwaka wa 2024. Putin ambaye  mbinu zake za kusalia uongozini  zimezua sifa na  lalama kutoka kwa wafuasi na wakosoaji wake ,amependekeza mageuzi makubwa ya kikatiba hatua iliyoifanya serikali nzima ya waziri mkuu  Dimitri Medvedev kujiuzulu siku ya jumatano.

Saa 24  baada ya hotuba ya Putin kuhusu  mpango wa kurekebisha katiba na mfumo wa uongozi wa urusi , Mikhail Mishustin aliyependekezwa kuwa waziri mkuu mpya ameidhinishwa na bunge la taifa hilo .

Mishustin  alipata kura  383 kati ya  424  zilizopigwa bila pingamizi na wabunge 41 wakijipeusha na kura hiyo. Kupandishwa  cheo kwa Mishustin ni sehemu ya mageuzi yaliyotangazwa jana na Putin  ambapo amepnedekeza rais kupewa maamlaka zaidi ya kuwezesha kuwafuta kazi maafisa wasiotekeleza kazi zao ipasavyo.