Ubalozi wa Amerika ,Nairobi umesema hoteli inayolengwa haijatambuliwa lakini ni mojawapo ya zinazopendwa na raia wa kigeni na wasafiri wanaokuja Kenya kwa biashara .
" Unafaa kuwa mwangalifu unapotembelea hoteli za Nairobi ,fahamu mazingira yako,Tathmini mikakati yako ya usalama na ufahamu utaratibu wa kuondoka katika eneo lolote wakati panapotokea dharura’ imesema sehemu ya ilani hiyo. Kulingana na msemaji wa Ubalozi huo Kenya na Marekani zinafanya kazi kwa ushirikiano ili kuchunguza hali ilivyo nchini . Ubalozi wa Amerika umesema ilani kama hizo zinawapa habari raia wake ili wafanye maamuzi yafaayo katika mipango yao ya usafiri . Ilani hiyo imejiri huku Inspketa mkuu wa Polisi Hillary Mutyambai akiwahakikishia wakenya kwamba idara yake ipo katika hali ya tahadhari ili kuwapa ulinzi .
Amesema polisi wameimarisha doria katika mipaka ya kuingia Kenya na wahalifu wenye nia ya kusababisha usumbufu watazuiawa kuingia nchini .
" Hata hivyo tungependa kuwatahadharisha wananchi kuwa makini zaidi hata polisi na vyombo vya usalama vinapoendelea na jitihada za kuwahakikishia usalama wao’ amesema Mutyambai kupitia taarifa .