Magavana wa Kaunti za Ukanda wa magharibi wakubaliana ishu ya ushuru

Magavana watano kutoka kaunti za ukanda wa magharibi kwa kauli moja wamekubaliana kuwa na (a common inter counties taxation) kwa minajili ya kushirikiana na kuruhusu wenyeji maeneo hayo kufanya biashara kwa uhuru.

Wakizungumza katika kaunti ya Bungoma baada ya kuwa na mkutano pamoja Magavana hao ambao ni Wycliffe Oparanya wa kaunti ya kakamega, Wilber Otichilo wa Vihiga , Sospeter Ojamong wa Busia , Khaemba Patrick wa Transnzoia naye Wickliff Wangamati wa Kaunti ya Bungoma wameelezea kuwa wana imani hatua hiyo ni mwanzo wa kuleta maendeleo katika maeneo hayo na nchi kwa ujumla.

Brian O. Ojama