Magoha kukutana na wadau huku pakiwa na kampeini za kutaka shule zifunguliwe

magoha 2
magoha 2
Waziri wa elimu George Magoha  ameitisha mkutano wa kushauriana na washka dau katika sekta ya elimu wiki ijayo  kujadil  mwongozo wa kufunguliwa kwa shule .

Mkutano huo utafanyika katika taasisi ya kustawishaji mtaala wa elimu  na utajadili tena suala tata la kufunguliwa kwa shule wakati huu wa janga la corona .

Mwezi julai ,wizara ya elimu   ilitangaza kwamba huenda shule hazitafunguliwa hadi januri mwaka ujao . Magoha hata hivyo  amesema uamuzi huo unaweza kubadilishwa  kulingana na jinsi kenya inavyokabiliana na janga la virusi vya corona .

Katika wiki moja  iliyopita kumekuwa na ongezeko la wito wa kufunguliwa kwa shule  huku wanaomiliki shule za kibinafsi  wakiitaka serikali kuzingatia kuzifungua shule mapema kuliko ilivyokuwa imetangaza hapo awali .

Hatua hiyo imetokana na kupungua kabisa kwa visa vya Covid 19 vinavyoripotiwa kila siku huku watu wengi pia wakipona ugonjwa huo na kurejelewa kwa shughuli za kawaida katika sekta nyingi za uchumi .

Rais Uhuru Kenyatta anatarajiwa kutoa mwongozo mpya  mwishoni mwa mwezi huu  kama sehemu ya mikakati ya kufungua uchumi ambao umelamazwa na janga hilo tangu mwezi machi mwaka huu .

Mnamo agosti tarehe 25  mzazi mmoja aliwasilisha kesi kortini akitaka kuishurutisha wizara ya elimu kuzifungua shule .

Shule zilifungwa mwezi machi  wakati Kenya ilipothibitisha kisa chake cha kwanza cha ugonjwa wa corona .

Mwenyekiti wa muungano wa wamiliki wa shule za kibinafsi Mutheu Kasanga amesema wanapinga pendekezo la kuwataka watahiniwa kurudia madarasa kwa mwaka mzima .