Majina Ya Ajabu Mombasani Na Asili Yake

1458707_10202823814210106_2064314729452327794_n
1458707_10202823814210106_2064314729452327794_n
Maeneo mengi nchini yamekua yakipewa majina ya ajabu ajabu lakini je unajua chanzo chake.  Kwa mfano katika eneo la pwani na hasa Mombasani utaskia eneo likiitwa steji ya Paka, Dongo Kundu, Mkanyageni, kuze na mengine mengi.

Jina Mkanyageni  ni la mtaa mmoja eneo la Old Town mjini Mombasa na kwa ufahamu wako pengine utafikiria linamaanisha kukanyaga mtu. Lakini  mtaalamu wa historia ya Pwani, Stambuli Abdulahi Nassir anasema jina hili linamaanisha - mtu anayekanya wageni au kitu kigeni, ndio huuitwa mkanya geni.

Nassir anasema  baadi ya majina kama Dungo Kundu , Steji ya Paka  yamekua yakidhaniwa kuwa na asili lakini ukweli ni kwamba  hayakuvumbuiwa kitambo .

Jina kama Toa Tugawe, watakwambia ni mtaa ambao ulikua na wezi wengi  kwa hivyo ukitoka safari zako na ukutane nao , baso watakwambia utoe ulicho nacho ili mgawanye.

Mtongwe ni kivuko kila mmoja anakifahamu sana. Lakini kwa mujibu wa Nassir hili sio jina moja bali mawili, Mto-Ngwe. Huu ulikua mto mdogo sana [mto] ambao kipimo chake kilikua kikipimika [ngwe].

Haya ni baadhi tu ya majina ya maeneo katika eneo hili,  Dunge Unuse,  Kadongo, Milango Saba, Floringi, Kadzandani, Mbuzi wengi na mengine mengi.

Je unafahamu majina ya ajabu katika eneo lako na asili yake? Yataje.