Watu 16 wamechangisha shilingi 49,490.
Hazina hiyo iliundwa mwezi aprili na muungano wa kuwasaidia wanawake wanaojishughulisha na biashara hiyo (Keswa) ambao hutetea pia maslahi ya wanaofanya ukahaba.
Kafyu imesababisha kuchukuliwa kwa hatua mbalimbali zinazoathiri shughuli za makahaba na hivyo basi kubana njia zao za kujipa kipato
"Wateja wengi wamezuiwa dhidi ya kuingia katika madanguro na wengi hawataki kuonekana mchana’ Shirika la Keswa limesema.
“ Sekta ya uchukuzi pia imezidisha nauli wakati huu wa janga la corona na kufanya kuwa vigumu kwa wanaofanya kazi za ukahaba kusafiri hadi kliniki za gharama ya chini kwa matibabu’
Wengi wao wameshindwa kupata pesa za kutibu maradhi yanayowakumba yatokanayo na virusi vya HIV na hivyo basi kuhatarisha maisha yao huku wengine wakifurushwa kutoka nyumba za kukodi kwa kushindwa kulipia.
Muungano huo amesema makahaba hutegema sana sekta ya jua kali kupata mapato na kuathiriwa kwa sekta hiyo pia kumevuruga shughuli zao .