Malkia Strikers watapata msaada kamili kutoka kwa serikali - Rais Kenyatta

malkia
malkia
Rais Uhuru Kenyatta amewahakikishia wachezaji wa timu ya taifa ya voliboli ya wanawake, Malkia Strikers, msaada kamili wa serikali wanapojiandaa na michezo ya Olimpiki ua Tokyo.

Rais aliipongeza timu hiyo kwa kuchukua nafasi pekee ya Kiafrika kwenye michezo hiyo ya msimu wa joto na akasisitiza kujitolea kwake  kuendelea kuwekeza katika michezo kupitia hazina ya michezo ya kitaifa.

“We have a fund now, a dedicated fund to promote our sports and culture. I want to make sure that money goes to these people who win the Olympics. We want money invested in our people, we want to see it used in these people who win gold medals for Kenya,” alisema.

Rais alitoa uhakikisho huo jana jioni wakati alipokutana na timu hiyo huko Mama Ngina Waterfront Kaunti ya Mombasa.

Ili kuhakikisha kuwa wanamichezo wa Kenya wanaendelea kuinua wasifu wa nchi hii kwenye hatua ya kimataifa, Rais alisema serikali itaendelea kuhakikisha wanariadha wa Kenya wanapata mapato mazuri kupitia talanta zao.

“We must come up with a policy that allows our sportsmen to focus only on sports. Those are the talents God gave them. I want them to know that one can focus on sports and earn a living through their talents,” rais alsema.

Hii ni mara ya kwanza Kenya itashiriki michezo hiyo kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 16 baada yao kufuzu bila kupoteza mechi yoyote katika michezo iliyo andaliwa Cameroon.

Akigundua kuwa wanamchezo ndio mabalozi wa mstari wa kwanza nje ya nchi, Rais alisema wanariadha wana nguzo kuu katika kuhakikisha umoja wa kitaifa.

“A lot of people know Kenya because of our gallant Kenyan sportsmen and women. Undisputedly, there’s one thing that makes us Kenyans, and that is our sports. When our sportsmen and women are out there, all Kenyans come together forgetting their petty differences,” alisema.

Rais alikuwa miongoni mwa mawaziri; Amina Mohamed (Michezo) na Najib Balala (Utalii).