Shughuli za kawaida zilisitishwa mtaani Oruba mjini Migori baada ya wakaazi wa mtaa huo kumpata mwanamke mwenye umri wa miaka 51 akiishi na mvulana mwenye umri wa miaka 17 kama mume wake .
Kakake mvulana huyo Erick Ochieng amesema amekuwa akimtafuta nduguye kwa muda akidhani kuwa amepatwa na ajali anapoendesha boda boda yake.
Alishangaa kujulishwa na wenyeji kwamba mvulana huyo alikuwa akiishi na mwanamke huyo katika nyumba yake . Wenyeji waliokuwa na ghadhabu walimpa kichapo mama huyo lakini alinusuriwa nma polisi .