Mambo yanayochangia sana Saratani mwilini - Emily Ochieng

Hii leo ndani ya ilikuwaje mgeni wetu amekuwa Emily Ochieng ambaye ni meneja wa Programme Kenya Cancer Assosiation.

Kulingana na Emily, ugonjwa wa Saratani uko katika nafasi ya tatu kwa magonjwa yanayoongoza kwa mauaji ya watu wengi kila siku. Ugonjwa wa saratani unasababisha vifo vya watu zaidi ya 90 kila siku hapa nchini Kenya.

 "Saratani ni hali ambayo hutokea wakati seli za mwili zinapokufa na badala ya kutolewa mwili, seli hizo huanza kumea tena kwenye viungo vya mwili. Jambo hili mambo yanayochangia sana Saratani mwilinii huletaa uozo kwenye meneo husika."

Ochieng anasema kuwa kuna aina mbili kuu za Saratani 'Screenable na Unscreenable'. Saratani zinazogundulika kwa haraka ndizo Screenable na mfano mzuri ni saratani ya Matiti na Saratani ya Koloni.

Kulingana naye Emily, Ugonjwa wa saratani husababishwa na ukosefu wa kufanya mazoezi mwilini, ukosefu wa vyakula vyote (balanced Diet). Ulaji wa nyama kwa wingi pia huleta ugonjwa wa saratani kwani nyama nyekundu huongeza mafuta mwilini.

 "Ubadilishaji wa maisha ni moja wapo wa mambo ambayo yamechangia katika ongezeko la saratani maishani hivi karibu hasa hapa nchini Kenya.
Tumekuwa tukila sana zile vyakula vya majokofu pamoja na vyakula vilivyoongezwa kemikali nyingi."

"Kila sehemu ya mwili inaweza kupata saratani na hivyo ningewaomba wakenya wafanyiwe uchunguzi kwani Saratani ikigundulika mapema inaweza kutibiwa," Emily anazidi kueleza.