Maneja wa KRA aliyekwepa kulipa kodi aachiliwa kwa dhamana Shilingi milioni 5

EACC
EACC
Maneja wa KRA r Joseph Gikonyo  na mkewe Lucy Kangai  wamekanusha  shtaka la kukwepa kulipa kodi  baada ya kufikisha mahakama siku ya Jumanne .

Wamedaiwa  kukosa kulipa kodi ya shilingi milioni 38,692,694   katika taehe tofauti kati ya mwaka wa 2010 na 2015  wakiwa momabasa kama wakurugenzi wa  Giche Ltd,  zilizofaa kutozwa kutoka kwa mapato yao pamoja na faini .

Wakili wa serikali   Annette Wangia  hakupinga kuachiliwa kwao kwa dhamana  lakini akaitaka mahakama kuangazia uzito wa mashtaka dhidi yao .

Hakimu  mkuu  Lawrence Mugambi  aliwaachilia kwa dhamana ya  shilingi milioni 5 pesa taslimu kila mmoja au bondi mbadala ya shilingi milioni 10

Maafisa wa  Tume ya maadili na kupambana na ufisadi  walimkamata Gikonyo siku ya jumatatu . EACC imekuwa ikimchunguza Gikonyo kwa mali ambayo hajaweza kueleza yenye thamani ya shilingi milioni 600 katika kipindi cha miaka mitano .

Afisa mkuu mtendaji wa EACC  Twalib Mbarak   kupitia taarifa amesema maafisa wa tume hiyo wamekuwa wakimchunguza afisa huyo wa zamani wa KRA pamoja , mkewe wake  Lucy Kangai   na kampuni yao ya biashara kwa jina  Giche Limited.