Mwanafunzi katika shule ya mseto ya Lumama huko Lugari amejiua baada ya kugundua kwamba mpenziwe wa kike ana mpenzi mwingine . Ripoti zaashiria kwamba mwanafuzi huyo wa kidato cha tatu alikunywa sumu baada ya mpenzi wake aliye katika kidato cha pili kugunduliwa kwamba ana mpenzi mwingine katika shule jirani .
Akithibitsha kisa hicho chifu wa eneo la lugari Evans Adavachi amesema mwanafuzi huyo aliamua kujiua baada ya kupata fununu kwamba msichana huyo alikuwa na uhusiano mwingine wa kimapenzi na mvulana wa shule jirani . Mvulana huyo aliaga dunia akipokea matibabu katika zahanati alikokimbizwa .