Mshambulizi wa Manchester United Marcus Rashford amesaini mkataba wa malipo ya £200,000 kwa wiki ili kusalia na kilabu hiyo hadi Juni mwaka wa 2023 ,akiwa na chaguo la kuongeza muda huo kwa mwaka mmoja zaidi .
Nyota huyo wa England mwenye umri wa miaka 21 alijiunga na United akiwa na umri wa miaka 7 na kusonga katika vitengo vya Oldtrafford hadi mwaka wa 2016 alipoichezea timu kuu akiwa na umri wa miaka 18 . Amesema Manchester United imemkuuza kama mchezaji na kama mtu huku akifurahia uamuzi wa kumpa mkataba mpya wa kuichezea the Red Devils .
" Nitafanya kila niwezalo ili kuifanya kilabu hii kurejelea hadhi yake na kuipa mafanikio ambayo mashabiki wetu wanastahili’ amesema Rashford.Mzaliwa huyo wa Wythenshawe Rashford ameichezea the Reds mechi 170 na kuiwakilisha England mara 32 .