Marriage Breakers? Jinsi wanawake 2 walivyowayumbisha Diamond na Harmonize

Wasanii wazito wa Bongo Diamond Platinumz na Harmonize wamejipata mashakani mwaka huu hasa baada ya kufanya video za nyimbo zao  mbili tofauti.

Katika video hizo waliwashirikisha wanawake wawili tofauti ambao wamekuwa na athari kubwa katika maisha yao .  Mrembo wa Re Union Malaika ambaye alihusishwa katika video ya wimbo Jeje amedai kuwa sababu ya Diamond kutengana na Tanasha . Ukweli kuhusu hilo haujajulikana lakini pamezagaa uvumi kwamba huenda Diamond alifanya uhusiano na kipusa huyo .

Hamornize na mke wake  Sarah pia wamejipata katika  msukosuko kwenye ndoa yao baada ya kudaiwa kwamba Sarah hajapendewa kuhusu picha nyingi za mume wake na  Kipusa Nicole Berry ambye yupo katika video ya wimbo ‘Bedroom’ ambao Hamornize ameufanya hivi karibuni .

Wasanii hao wawili wamejipata katika matatizo ya mahusiano yao kwa ajili ya warembo waliohusishwa katika video zao .Je,katika muziki ,mpaka na upi kati ya kazi na maisha yako binafsi?

Kutokana na ushahidi katika mitandao ya kijamii ,Hamornize ndiye aliyeanzisha vita kati yae na mkewe .Katika posti moja ,aliashiria kwamba yeye na Nicole wangekuwa Couple nyingine kali sana endapo angekuwa single.Aliandika ;

 ILA HIZI KAZI ZETU MUNGU NDIO ANATULINDA….!!!!!! NDIOMANA NIKAOGA MAPEMA HIVI NINGEKUWA SINGLE HUYU DADA INGEKUWAJE UNADHANI..??

Jiongoe kwa picha zao hapa,Nicole aliyeshirikishwa katika Video ya Bedroom ya Hamornize na  Malaika aliyeshirikishwa katika Video ya Jeje ya Diamond