Maseneta 25 wakula njama ya kuyakataa mapendekezo ya Uhuru na Raila

Rais Uhuru Kenyatta na kiongozi wa ODM Raila Odinga wapo katika hatari ya kufadhaishwa tena na maseneta ambao wamepa kuyakataa mapendekezo yao kuhusu  mfumo unaotumiwa kugawa pesa za kaunti .

Hili limeibuka katika mkutano uliofanyika jumatatu kati ya uongozi wa senate ,hazina ya kitaifa na wdau wa ugatuzi ili kuidhinisha kutolewa kwa shilingi bilioni 187 kuzuia kullemazwa kwa oparesheni za serikali za kaunti baada ya utata kuzuka kuhusu fumo unaotumiwa kagawa pesa hizo .

Gazeti la The Star limegundua kwamba maseneta 25  ambao wiki jana waliongoza kuangushwa kwa mswada wa serikali kupuitisha mfumo huo  pamoja na marekebisho yaliyopendekezwa  wanapanga tena kuyakataa mapendekezo yaliyotolewa ili kumaliza utata huo .

Marekebisho  hayo yametolewa na kiranja wa wengi katika senate aliyeungwa mkono na rais Kenyatta na Kiongozi wa ODM Raila Odinga .

Wakiwa ni maseneta 25 wanaopinga  marekebisho hayo ,maseneta hao wamezidi idadi ya maseneta 24 waaohitajika  kukataa mfumo huo  ambao utazifanya kaunti 18 kupiteza jumla ya shilingi bilioni 17

Utata huo sasa umejaa sarakasi za kisiasa  huku naibu wa rais William Ruto akiwashawishi wafuasi wake kuukata mfumo huo .

Siku ya jumapili  Raila alikuatana na  baadhi ya washirika wa Uhuru  wakiongozwa na naibu mwenyekiti wa chama cha Jubilee David Murathe  nyumbani kwa katibu mkuu wa COTU Francis Atwoli .

Katika mkutano huo Raila aliwahakikishia washirika hao wa rais kenyatta kwamba mrengo wake utaunga mkono mfumo huo .

Seneta wa Siaya James Orengo  ambayeni kiongozi wa wachache katika senate  alipewa jukumu la kuhakikisha kwamba kundi la Odinga linatekeleza matamnio yake kuhusu kura  ya mfumo huo