Mashabiki wa Radio Jambo watuzwa na Sonko wa Masonko.

NA ABRAHAM KIVUVA

Kituo chako mahabubu cha Redio Jambo kimeratibisha mchakato na mpango mzima wa kuwatunuku wasikilizaji na mashabiki sugu kwa zawadi kemkem mwezi huu wa Julai na Agosti.

Pia soma:

Kupitia swali mboga sana la kuitambua “the phrase that pays”, msikilizaji anatuzwa shilingi elfu moja. Kwa kutengeneza bango na kuandika radio jambo ongea usikike, mshindi anatuzwa elfu 5 pesa taslimu.

Mashabiki wa kutoka sehemu za ukambani na maeneo ya Taita taveta watapata nafasi adimu zaidi kuonana macho kwa macho na sonko wa radio Jambo juma lijalo.