' Masomo ya Nyumba Kumi ': Walimu kutoa mafunzo wakati wa janga la Covid 19-Magoha

Magoha
Magoha
Walimu watatoa mafunzo kwa wanafunzi kupitia mfumo kama ule wa nyumba kumi  ,amesema waziri wa elimu George Magoha .

Akizungumza na n waandishi  wa habari siku ya alhamisi katika makao makuu ya KICD  Magoha amesema  kundi  la maafisa kutoka mashirika mbali mbali  ya serikali litaunda mwongozo na mikakati ya kuwawezesha walimu kutoa mafunzo ya kijamii  kwa wanafunzi .

" walimu watawapa wanafunzo masomo kuhusu  uadilifu chini ya  muundo wa nyumba kumi . TSC iatoa mpango huo ambao hautawagharimu wazazi chochote’ amesema Magoha

Katika elimu ya msingi , wadau katika sektaya elimu wamesema licha ya mafunzo kutolewa kwa njia ya redio ,runinga na kupitia mtandao ,kuna wanafunzi wengi ambao hawawezi kuyapat mafunzo hayo .

Wizara ya elimu  na TSC  zikitumia kundi la pamoja na idara mbali mbali za serikali  pamoja na machifu sasa litatumia   mpango wa Nyumba kumi ili kufanikisja masomo hayo ya ‘kijamii’

mpango wa Nyumba Kumi  ulianzishwa kupitia agizo la rais  na kuwekwa katika gazeti rasmi la serikali kama njia moja ya kukabiliana na ukosefu wa usalama wakati visa vya ugaidi na uhalifu vilipoongezeka mwaka wa 2013.

Magoha ameongeza kwamba vyuo vingi vikuu na vya mafuzoya elimu ya juu haviko tayari kufunguliwa  na vitaslaia kufungwa hadi januari mwaka wa 2021 . Ameongeza kwamba serikali imetenga fedha za kuwalipa walimu walioajiriwa na bodi za shule ,maafuisa wa ulinzi na kulipa gharama kama vile maji na umeme katika shule za umma