Mateka wa Moi!;Watu mashuhuri waliotiwa kizuizini na rais Mstaafu hayati Moi

Rais mstaafu hayati Daniel Arap Moi aliaga dunia mnamo Februari mwaka huu huku wengi wakimkumbuka kwa njia mbalimbali, Moi alizikwa mnamo tarehe 12/02/2020 nyumbani kwake Kabarak Nakuru.

Wakati  Moi alipokuwa mamlakani uongozi wake ulikuwa wa kupigiwa mfano, kwa sababu hangewacha mwenye makosa akae na makosa hayo bali alikuwa anawahadhibu ipasavyo.

Baadhi ya watu waliotiwa kizuizini wakati wa uongozi wa hayati Moi ni hawa hapa;

Wakili John Khaminwa

John ni wakili katika mji wa Nairobi, aliponea chupuchupu baada ya kuandamwa hadi kwa boma lake na helkopta ya wanajeshi mnamo juni 4/1982 na kufikishwa katika afisi kuu za CID na kuachiliwa  mnamo oktoba 12/1983.

Raila Amolo Odinga

Mwaka wa ,1983 aprili,14 Raila alitiwa kizuizini na watu wengine na kunakili yote yaliyopitiwa wakiwa ndani.

Maina wa Kinyatti

Juni,7,1982, mhadhiri wa chuo kikuu alikamatwa kwa uchapishaji  taarifa za  uchochezi. alifungwa kwa miaka sita kwa kosa hilo.

Kamoji Kang’aru Wachira na Edward Akong’o Oyugi

Mwaka wa 1982,Julai,24 wahadhiri hao wawili walitiwa kizuizini, walikuwa wahadhiri katika chuo kikuu cha Nairobi

Wachira alifunza jiografia naye Edward alifunza somo la saikologia katika chuo hicho.

Koigi wa Wamwere

Alikuwa mbunge wa Nakuru alipotiwa mbaroni agosti,12,1982 kwa kuwa katika kikundi ambacho kilifahamika kama 'Six Bearded Sisters'

Kenneth Matiba

Ni mwanasiasa ambaye alipatwa na ugonjwa wa papasa baada ya kufungwa gerezani wakati wa uongozi wa Moi kutokana na msimamo wake wa kukashifu uongozi uliokuwepo wakati huo uongozi uliotajwa kama wa kikoloni.

Alikuwa gerezani 1990 Julai.

Kwa hakika Moi alifanya kazi yake kwa ustaarabu wake na mwelekeo mwema.