Matukio na Habari Muhimu Toleo la Saa saba Jumatatu 14th Oct 2019

RADIO JAMBO MIC
RADIO JAMBO MIC
 

Video ya dakika 47  iliyorekodiwa   ya Peter Ngugi aliyekuwa akiwapasha polisi habari  akikiri kuhusika na mauaji ya wakili Willie Kimani  haitachezwa kortini .jaji  amesema  afisa aliyerekodi video hiyo  hakufutwa kanuni zifaazo wakati wa kuichukua video hiyo iliyofaa kutumiwa kama ushahidi .

Miili ya  wakenya walioaga dunia  katika ajali ya ndege  ya  shirika la Ethiopia  airlines imewasili katika uwanja wa ndege wa JKIA  ili kuchukuliwa  na jamaa zao .miili 28 kati ya 32 ya wakenya  hao walioafriki katika mkasa huo imewasili mapema  leo katika uwanja huo  .watu 157 waliangamia katika ajali hiyo mwezi machi .

Uhaba wa walimu huko taita taveta unachangia kudorora kwa ubora wa elimu  .mbunge wa mwatate  Andrew Mwadime  aniataka tume ya kuwajiri walimu TSC  kuwaajiri walimu zaidi  katika eneo hilo kwani kuna vijana wengi waliohitimu kuwa walimu lakini hawana kazi .

Mbunge wa kitui  mashariki Nimrod Mbai  anataka kamishna wa kaunti ya Kitui John Ondego ahamishwe kwa  madai ya kukosa kurejesha hali ya usalama katika eneo hilo  linaloshambuliwa mara kwa mara na wafugaji wa ngamia . Mbai amesema wenyeji sasa wamelazimika kuishi katika kambi za muda  ilhali serikali haijachukua hatua zozote madhubuti za kuwalinda .Odengo hata hivyo amekana kuwyatelekeza maslahi ya wakaazi hao.

Chama cha ODM kimetakiwa kuwahakikishia wakenya kwamba kitadumisha amani wakati wa uchaguzi mdogo wa kibra .mbunge wa  kiharu Ndindi Nyoro  amesema kisa kama  kilichotokea mwishoni mwa wiki ambapo msafara wa mgombeaji wa Jubilee Mcdonald mariga ulishambuliwa kwa mawe  sio jambo linalofaa kukubaliwa .

Serikali itazidisha mara dufu jitihada za kukabiliana na udanganyifu katika mitihani ya kitaifa mwaka huu .afisa mkuu mtendaji wa  baraza la kitaifa la mihani Mercy Karogo  amewashauri  maafisa wakuu wa elimu katika kaunti ndogo kuhakikisha kwamba  wanafuatilia kikamilifu   usimamizi   wa zoezi la mtihani katika maeneo yao .

Wakaazi wa Mombasa wanaitaka serikali kuboresha usalama katika feri  ili kuzuia maafa siku za usoni . wamesema baadhi ya  sehemu za feri zinafaa kuboreshwa na pia kuweka vifaa vya kuwawezesha watu kujiokoa wakati panapotokea  dharura .