Matumaini Feki: Tanzania yaonywa dhidi ya kuwapa wananchi matumaini butu kuhusu coronavirus

MAGUFLI
MAGUFLI
Kiongozi wa upinzani Tanzania Zitto Kabwe  ameionya serikali ya nchi hiyo dhidi ya kuwapa wananchi matumaini   ya uongo kuhusu vita dhidi ya virusi vya Corona  huku visa vya ugonjwa huo vingeozeka.

Kabwe amesema wananchi wanafaa kuambiwa ukweli kuhusu taswira hasili ya jinsi mambo yalivyo. Taifa hilo lilisajili visa 30 zaidi siku ya Jumatano na kufikisha jumla ya visa 284 vya watu walio na coronavirus

Waziri mkuu wan chi hiyo  Kassim Makaliwa  Jumatano aliwarai wananchi kuiamini serikali  na wataalam wake wa afya katika vita dhidi ya ugonjwa huo. Majaliwa alisema  serikali mwanzo itatathmini hatua zifaazo kabla ya kuamua kutangaza mikakati  kabambe ya kuweza kuzuia usambaaji wa virusi hivyo. Mikutano na misongamano ya watu katika hafla za kidini bado imeruhusiwa  na rais Magufuli amenukuliwa akisema kwamba virusi vya Corona haviwezi kufaulu katika mwili wa kristu na kuwahimiza watu kufanya sala na maombi

Rais Magufuli amefutilia mbali uwezakano wa kutoa tangazo la kutotoka nje  katika mji mkuu wa kibiashara  Dar es Salaam  ambako visa vingi  vya ugonjwa huo vimeripotiwa.

Amesema tangazo kama hilo litavuruga kabisa uchumi katika jiji hilo la bandari linalotegemewa kwa kiasi kikubwa cha pato la nchi