Mauaji ya watu 3 chini ya saa 12 yatamausha Gilgil

Wakaazi wa  mtaa wa hospitali ya kaunti ndogo ya Gilgil  wametamaushwa na  mauaji ya watu watatu katika hali ya kutatanisha chini ya saa 12  baada ya watoto wawili kuuawa kwa kupwa sumu iliyotiw akwenye machungwa  na muuguzi mmoja kudungwa kisu hadi kufa .

Watoto hao wawili wanadaiwa kuuwa na mwanamke jirani ambaye aliwapa machungwa yaliytiwa sumu siku ya jumatatu .mwanamke huyo amekamatwa na kiini cha kufanya hivyo hakijajulikana .

Muuguzi  mmoja naye aliauawa katika nyumba za wafanyikazi wa hospitali hiyo siku ya Jumanne baadaya mume wake kumdunga  kisu mara 13  kisha baadaye mshukiwa akajisalimisha kwa polisi .

Visa hivyo viwili vimewashangaza majirani  .wafanyikazi wa kutoa huduma za ushauri na viongozi wa makanisa wamezua hofu kuhusu ongezeko  la ghasia na dhulma za kinyumbani wakati huu wa janga la corona .

OCPD wa Gilgil John Onditi amesema jirani ya watoto hao wawili amekamatwa  na andiye aliyekuwa mtu wa mwisho kuonekana nao  na imebainika kwamba aliwapa sumu .

Kuhusiana na mauaji ya muuguzi aliyetambuliwa kama Josphine Kamau  OCPD  amesema  mume wakeanayeripotiwa kuwa mkritu aliyeokoa alijaribu kujiua na alikuwa chini ya matibabu .

Onditi  amesema wawili hao waligombana na mwanamme huyo ambaye ana duka la kuuza vitabu katika eneo la Nyandarua alimuua mkewe kwa kumdunga kisu mara 13.

“ Baada ya kutekeleza mauaji hayo mwanamme huyo alijaribu kujiua  na anapokea matibabu kisha atafikishwa mahakamani’ Onditi amesema

Jirani ambaye hakutaka kutajwa amesema mwanamme huyo alishuku mkewe alikuwa na uhusiano na mmoja wa rafiki zake .