Kwa mujibu wa marekebisho hayo yanayopendekezwa na mbunge huyo wa suba kusini , unafaa kutangaza katika kipindi cha wiki mbili ulikotoa pesa hizo baada ya kuzitoa wakati wa hafla ya kutoa mchango .
Amesema pendekezo hilo jipya litasaidia kumaliza mtindo wa sasa wa wanasiasa na watumishi wa umma kutoa kiasi kikubwa cha pesa katika hafla za michango ambapo baadaye hugunduliwa kwmba fedha hizo zimepatikana kupitia njia za ufisadi na uporaji wa pesa za umma .
Mbadi anataka kurekebisha sehemu za 13, 26, 28 na d 30 za sheria ya wafanyikazi wa umma ya mwaka wa 2003 ili kuhakikisha kwamba pesa zilizopatikana kupitia njia za ufisadi hazitolewi katia harambee na kuwafumba macho wapiga kura .
Kumekuwa na majibizano miongoni mwa wanasiasa kuhusu hatua ya baadhi yao kuonyesha kiasi kikubwa cha pesa ambazo huzitolewa katika michango na hasa kwa makanisa . Naibu wa rais William Ruto amekuwa mstari wa mbele katika hafla kama hizo na marekebisho hayo ya Mbadi yanaonekana kumlenga . Ruto kwa upande wake ameshikilia kwamba anafahamu alikotoka katika ufukara na hivyo basi ataendelea kutoa msaada wa pesa kwa wakenya wanaohitaji usaidizi .
Suala hilo la michango na pesa zinazotolewa na wanasiasa limekuwa kubwa katika mijadala ya kampeini za uchaguzi mkuu ujao wa mwaka wa 2022 .