Haya yanajiri pindi tu baada ya msanii huyo kuzua rabsha bungeni, Jumanne mchana kwa kuingia akiwa amevalia sketi fupi.
Hapo ndipo walinda lango pamoja na wengi waliokuwa bungeni wakabaki wameduwaa na kumzuia asiingie hoteli iliyo bungeni.
Sankok alisema kuwa alipoenda kumchukua Akothee katika lango kuu la bunge alimuangalia na kudhibitisha kuwa alikuwa amevaa vyema. Licha ya hilo, anasema alipofika bungeni hapo ndipo aliambiwa kuwa sketi yake lazima iwe chini ya magoti.
Sankok alieleza,
Mbona niombee msamaha kwa kumleta mkenya mrembo mwenye miguu mirefu ili awaalike wabunge wenzangu waweze kumuunga mkono na kuchangia mipango yake ya kusaidia wanaoumia, Turkana.
Akothee alikuwa amevalia vyema zaidi kwani alikuwa amevalia mavazi rasmi.
Nilipoenda kumchukua katika lango kuu nilimchambua kutoka pembe zote na alikuwa amevalia vyema, lakini nilipofika hapa wakasema kuwa sketi yake lazima iwe chini ya magoti.