Mbunge wa Matayos atishia kuishtaki serikali na inspecta mkuu wa polisi

Geoffrey Odanga
Geoffrey Odanga
Mbunge wa Matayos Kaunti ya Busia Geoffrey Odanga ametishia kuishtaki serikali na inspector mkuu wa polisi Joseph Boinet kutokana na visa vya maafisa wa polisi wa kituo cha kampuni ya miwa ya Busibwabu ya kuwavamia na kuwaumiza wananchi wasio kuwa na hatia kwa kizingizio cha kupiga vita pombe haramu.

Odanga amewataka maafisa hao kubadili tabia yao au waondolewe eneo hilo.