Mbunge wa Starehe Jaguar akamatwa na polisi

Mbunge wa starehe Charles njagua  kwa jina maarufu jaguar  amekamatwa kufuatia matamshi yake ya kuwachochea wafanyibiashara wa eneo bunge lake dhidi ya wenzao kutoka nchi za kigeni .  Jaguar  amekamatwa  baada ya kukosa kujisalimisha katika kituo cha polisi cha bunge.

 Mkusanyiko wa Habari zaidi 

 Itakuwa afueni wa wadhamini wa mikopo  endapo mswada unaolenga kuwalinda utapitishwa kuwa sheria  .mswada huo uliopendekezwa  na mbunge wa juja Francis waititu  unapendekeza kwamba  aliyetia sahihi kudamini mkopo wa mtu hafai kupokonywa mali yake kwa haraka endapo njia zote hazijatumiwa kumfanya aliyekopa pesa kuzilipa kwanza .

Serikali imejitenga na matamshi ya mbunge wa starehe  Charles kanyi kwa jina la usanii jaguar kwamba wafanyibiashara wa kigeni  walioko jijini  wanafaa kurejeshwa makawao .  jaguar alinaswa katika video akitoa vitsho vya kuwaongoza wafanyibiashara wa hapa Nairobi kuwaondoa wenzao kutoka nje za kigeni .tayari bnge la taifa jirani la Tanzania limelalamikia vikali matamshi hayo .

Wanaharakati wa kupambana na saratani chini ya vugu vugu la  Network of Cancer organizations  wamesema  madai ya madai ya madakari wa kanis aa katoliki kwamba chanjo cha HPV itaongezwa visa vya ugonjwa huo  yanapotosha . mwenyekiti David Makumi amesema uchunguzi wa kina umeonyesha kwamba chanjo hiyo  huzuia ukuaji wa chembe za virusi hivyo HPV na hivyo basi  njia bora kuzuia  ugonjwa huo .

Wakenya katika maeneo ya mashinani wataweza kupata matokeo ya vipimo vya kiwango cha virusi  vya HIV katika   muda wa dakika 70  baada ya kuidhinishwa kwa  vifaa  rahisi vya kubebwa vya kupima vilivyotolewa na shirika la WHO . Hapo awali sampuli zilichukuliwa na kupelekwa kwa shirika la kemri  na matokeo kutolewa baada ya wiki mbili . vifaa hivo vya WHO kwa jina M-PIMA vitawasaidia wakaazi wa maeneo ya mbali huko mashinani .

Peter Mbithi  atafahamu hatma yake leo baada ya kuonyesha nia ya kutaka kuendelea kuhudumu kama mhadhiri mkuu wa chuo kikuu cha Nairobi .Baraza la chuo hicho linaloongozwa na Julia Ojiambo litafanya uamuzi wake leo .hatamu ya Mbithi  inafika tamati januari mwakani .

Mshukiwa mmoja wa ujambazi ameuawa kwa kupigwa risasi na polisi katika eneo la jomvu  huko Mombasa . Polisi walifahamishwa na wakaazi  kwamba mshukiwa huyo alikuwa  akilimiki bunduki kinyume cha sheria na wakaanza kumchunguza .  Alianza kuwafyatulia risasi polisi walipompata nyumbani kwake .

Kenya leo inajiunga na ulimwengu kuadhimisha siku ya kupambana na matumizi ya dawa za kulevya na ulanguzi wa mihadarati .kauli mbiu ya maadhimisho ya siku hii mwaka huu ni  ‘afya kwa  haki na haki kwa afya’. Umoja wa mataifa umesema kauli mbiu hiyo inawiana na maazimio ya kukabiliana na mihadarati kwa njia ya jumla kuhusisha  afya ,haki  na  taasisi ya huduma za kijamii .