Mchakato wa kuwatafuta watu waliotangamana na mwathiriwa wa virusi vya Corona Trans -Nzoia umeanza

BOTWA-GIRL-730x414
BOTWA-GIRL-730x414
Wahudumu wa afya kaunti ya Trans Nzoia wameanza harakati za kuwatafuta watu waliotangamana na msichana wa miaka 15 aliyepatikana na virusi hivyo baada ya kufanyiwa vipimo.

Msichana huyo inasemekana kuwa alisafiri kutoka kaunti ya Mombasa akiwa na wazazi wake hadi kijiji chao Botwa ,Karara  kaunti ya Trans Nzoia Mashariki.

Haijabainika wazi ni kwa nini msichana huyo hakuwekwa chiuni ya karantini kwa siku 21 baada hya kuwasili eneo hilo.

Yamkini kulingana na taarifa za wahudumu wa afya hao wanasema kuwa mwathiri amekiri kutangamana na ndugu zake wawili ambao kufikia sasa wamewekwa kwenye karantini kwa siku 14.

Shughuli za kuwatafuta waliotangamana naye sasa zimeanza rasmio hii leo.

Kunngti hiyo kufikia sasa imkesajilio kisa kimoja tu cha maambukizi ya corona kulingana na takwimu za wizara ya afya  hiyo jana.

Kufikia sasa Kenya imesajili visa 1192 vya maambukizi ya virusi baada ya watu wengine 31 kupatikana.