Messi The great: Ashinda tuzo ya 7 ya golden Boot katika La Liga

Lionel Messi  ameshinda tuzo yake ya saba ya mfungaji wa mabao mengi katika La liga  na yake ya nne mfululizo baada ya kuifungia Barcelonamabao mawili katika ushindi wao wa  5-0 dhidi ya kilabu ya  Alaves  katika siku ya mwisho ya ligi hiyo ya uhispania .

Nahodha huyo wa Barcelona alimaliza kwa mabao 25  ,manne mbele ya mshambuliaji wa Real Madrid Karim Banzema . mchuano huo hata hivyo haukuwa muhimu wa Barca kwani tayari walikuwa wameshalinyakua taji hilo siku ya alhamisi .

Messi  alifaulu kumkanganya mlinda lango ili  kufunga mabao mawili huku  Ansu Fati, Luis Suarez na  Nelson Semedo  wakifunga mabao mengine .

Riqui Puig, Messi  na Arturo Vidal wote waligonga mkuti kabla ya Fati kufungua mwanzo wa mabao .

Hii ndio ya kwanza  kwamfungaji bora wa La liga kufunga chini ya mabao 30  tangu  nyakati za Daniel Guiza wa Mallorca miaka 12 iliyopita .