Mfalme wa Thailand Maha Vajiralongkorn, aka Rama X ameripotiwa kujifungia kwenye karantini na wanawake 20 umbali wa kilomita zaidi ya elfu nane kutoka nyumbani.
Taifa hilo limesajili visa 1,651 huku visa 17 vikisajiliwa Jumanne pekee na watu 10 wakiaga dunia kwa ajili ya coronavirus. Kiongozi huyo mzushi amekuwa akijitenga katika hoteli moja ya kifahari katika mji wa Garmisch-Partenkirchen na ujumbe wake, jarida la limeripoti.
Mfalme huyo pamoja na msafara wake wamechukua hoteli nzima ya Grand Hotel Sonnenbichl baada ya hoteli hiyo kupata idhini ya kuruhusu msafara wake. Miongoni mwa walioandamana naye ni wanawake 20 wa kumpa raha zake na wafanyikazi kadhaa.
Gazeti la ujerumani Bild, limesema hadi sasa haijafahamika iwapo wake zake wanne pia wapo katika hoteli hiyo.
MHARIRI: DAVIS OJIAMBO