Mhudumu wa boda boda Uganda ajiteketeza baada ya ‘kuitishwa hongo’

hussein
hussein
Mhudumu mmoja wa boda boda nchii Uganda aliye na umri wa miaka 29 ameaga dunia baada ya kujitia moto  ndani ya kituo cha polisi .

Pikipiki ya Hussein Walugembe ilinaswa na polisi katika wilaya ya masaka siku ya jumatatu  na  akatakiwa kulipa rushwa ya takriban shilingi elfu 4  ili arejeshewe lakini hilo halikumfurahisha .idara nzima ya trafiki katika eneo hilo sasa ipo chini ya uchunguzi kwa mujibu wa  msemaji mmoja wa polisi .

Pia inaripotiwa kwamba  Walugembe  alikuwa akiishi katika makaazi ya polisi na alikuwa akiwazuia maafisa hao chakula . Nchini Uganda usafiri wa boda boda umepigwa marufuku  katika baadhi ya nyakati  ili kuzuia  maambukizi ya virusi vya corona na mara kwa mara polisi hufanya msako wa kuwakamata wahudumu wanaokaidi marufuku hiyo .

Wahudumu hao wanaruhusiwa kufanya kazi zao kuanzia saa kumi na mbili alfajiri na  hadi saa kumi na moja jioni na  wanaweza tu kusafirisha mizigo .

Polisi wanasema  Walugembe  alikuwa amempa rafiki yake pikipiki yake aliyepatikana akimsafirisha abiria hatua iliyosababisha kunaswa kwa pikipiki hiyo . Baadaye alifadhaishwa na kutibuka kwa  juhudi zake kutaka pikipiki yake iachiliwe  ndiposa akaamua kujifungia katika chumba kimoja ndani ya kituo cha polisi na kujiteketeza kutumia  mafuta petrol aliokuwa ameficha kweye chupa .