Mashindano hayo ya kila mwaka yalikuwa yameratibiwa kuanza kufanyika Agosti 14 hadi 24 katika kaunti ya Kakamega japo mkutano ulioandaliwa kati ya International Sports Federation ukiongozwa na rais wake Laurent Petrynka na katibu mkuu wa shirika la FEASSSA secretary David Ngugi uliamua kuafikia kufanyika kwa mashindano hayo mwaka ujao.
Ngugi ambaye pia ni katibu mkuu wa shirikisho la michezo ya shule za upili humu nchini Kenya Secondary School Sports Association (KSSSA), alisema kuwa itakuwa vigumu kufanyika kwa mashindano hayo mwaka huu kutokana na virusi hivyo.
“We’ve made a decision to postpone the championship until next year because of the health challenge the world is facing. Kenya remains the host of the postponed games and it will be bigger next year because the ISF president has promised us he will attend. Also, the president has said that ISF has rescheduled the World Games to next October, ” Ngugi .
Kwa upande wake mwenyekiti wa shirika la ISF Petrynka amesema watashirikiana na mataifa husika katika mashindano hayo ili kuhakikisha kuwa wanapigana na virusi hivyo hatari.