logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mtoto aliyelia kukutana na CR7 hatimaye akutanishwa naye - video

Ronaldo alikuwa na mazungumzo ya kirafiki na Adrian, akampa shati yenye autograph yake na kupiga picha.

image
na Davis Ojiambo

Michezo20 September 2023 - 08:35

Muhtasari


  • • Mkutano huo ulifanyika kabla ya mechi ya ufunguzi ya Ligi ya Mabingwa ya timu ya Saudi Arabia dhidi ya Persepolis ya Iran.

Mcheza soka maarufu wa klabu ya Al-Nassr ya Saudi Arabia Cristiano Ronaldo alivutia idadi kubwa ya mashabiki alipowasili katika mji mkuu wa Iran siku ya Jumatatu kabla ya kuchuana na Persepolis, lakini miongoni mwa umati wa watu waliojitokeza nje ya hoteli yake pekee ni kijana mdogo aliyetambulika kwa jina Adrina.

Mashabiki hao walifurika nje ya hoteli hiyo kwa lengo la kumuona Ronaldo lakini hawakuweza kumuona na kijana huyo mdogo alionekana akilia kwa uchungu kwa kukosa nafasi muhali ya kukutana na mchezaji ambaye anampenda na kumuenzi.

 Kwa mujibu wa jarida la Iran Front Page, Adrian, ambaye kilio chake nje ya hoteli ya Espinas Palace ya Tehran kwa kutoweza kukutana na Ronaldo kilisambaa, alitambuliwa na maafisa wa klabu hiyo ya Saudia na kupelekwa kwenye chumba cha mchezaji huyo.

Ronaldo alikuwa na mazungumzo ya kirafiki na Adrian, akampa shati yenye autograph yake na kupiga picha.

Kijana huyo alikuwa akivalia jezi ya Al-Nassr yenye jina la Ronaldo mgongoni na kuingizwa kwenye chumba ambacho supastaa huyo wa Ureno alikuwa akisubiriwa. Ronaldo alipiga picha na kusaini jezi ya mtoto huyo.

Mkutano huo ulifanyika kabla ya mechi ya ufunguzi ya Ligi ya Mabingwa ya timu ya Saudi Arabia dhidi ya Persepolis ya Iran mjini Tehran siku ya Jumanne. Kikosi cha Ronaldo kiko kwenye mbio za kushinda mechi tano kuelekea sare.

"Haya! habari yako?" Ronaldo aliuliza mvulana huyo alipoingia chumbani. "Uko vizuri? Nikumbatie!"

Shabiki huyo mchanga hata alionyesha hisia zake kwa sherehe maarufu ya bao la Ronaldo.

Al-Nassr wanatarajia kuanza kampeni yao ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa nguvu. Wako katika kundi lenye Persepolis, Al-Duhail na Istiklol.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved