logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Aliyekuwa kiungo wa Nigeria Jay Jay Okocha asherehekea miaka 25 kwenye ndoa

Video kutoka kwa tukio hilo la kushangaza zilivutia watu wengi, zikiangazia mitandao ya kijamii.

image
na Davis Ojiambo

Michezo23 October 2023 - 09:13

Muhtasari


  • • Watoto wao wawili wa kupendeza, Ajay Okocha na Daniela Okocha, pia walikuwepo kushiriki furaha yao.
Jay Jay Okocha

Kiungo wa kati matata wa timu ya taifa ya Nigeria miaka ya 90 na mapema 2000s Jay Jay Okocha alifanya tafrija ya kipekee kusherehekea kufikisha miaka 50 na pia kusherehekea miaka 25 kati ya hiyo akiwa ndani ya ndoa na mkewe, Nkech.

Mkwasi huyo wa kupiga chenga za kimaudhi alisherehekea matukio haya mwili kwa pamoja katika mji wa kimahaba wa Maldives kwa karamu iliyoenea mitandaoni.

Video kutoka kwa tukio hilo la kushangaza zilivutia watu wengi, zikiangazia mitandao ya kijamii.

Wawili hao walionekana wakirejesha viapo vyao katika hafla ya kugusa hisia ambapo walionekana kustaajabisha wakiwa wamevalia vazi jeupe la kitamaduni la arusi.

Katika video nyingine ya kusisimua, mke mrembo wa Jay Jay Okocha, Nkechi, alivalia gauni maridadi jeusi huku wawili hao wakicheza kwa furaha karibu na kila mmoja.

Watoto wao wawili wa kupendeza, Ajay Okocha na Daniela Okocha, pia walikuwepo kushiriki furaha yao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved