logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Michael Olunga ana kwa ana na Ronaldo na Mane Jumanne usiku kwenye Champions League

Timu iliyo katika nafasi ya kwanza pekee ndiyo itafuzu baada ya kumalizika kwa hatua ya makundi.

image
na Davis Ojiambo

Michezo24 October 2023 - 07:32

Muhtasari


  • • "Unapomzungumzia Cristiano Ronaldo, unamzungumzia mmoja wa wachezaji bora zaidi duniani," Olunga alimpa maua Ronaldo.
Olunga na Ronaldo

Ligi ya mabingwa katika vilabu vya mataifa ya bara Asia itaendelea usiku wa leo Jumanne ambapo timu ya nahodha wa Kenya, Michael Olunga, Al Duhail ya Qatar itasafirisha kwenda nchini Saudi Arabia kuchuana na timu ya nahodha wa Ureno Christiano Ronaldo, Al Nassr.

Mchezo huo utakaopigwa kwenye Uwanja wa Al Awal Park Oktoba 24, utakuwa ni mchezo wa tatu wa hatua ya makundi kwa pande zote mbili huku mbio za kuwania kufuzu kwa raundi inayofuata zikipamba moto.

Kwa sasa Al-Nassr ya Ronaldo inaongoza kundi hilo la timu nne ikiwa na pointi 6 baada ya kuzishinda Persepolis na Istiqlol Dushanbe. Al-Duhail, bado hawajashinda mchezo wowote baada ya kutoka sare na Istiqlol kabla ya kushuka dimbani Persepolis. Wanashika nafasi ya tatu kwenye msimamo.

Timu iliyo katika nafasi ya kwanza pekee ndiyo itafuzu baada ya kumalizika kwa hatua ya makundi.

Upande wa Al Duhail wanajivunia talanta kama Olunga na Phillipe Coutinho huku wenzao Al Nassr wakijivunia mastaa kama Ronaldo na Mane miongoni mwa wengine.

Akizungumza na vyombo vya habari kuelekea mpambano wa leo, Olunga alimmiminia sifa Ronaldo lakini akasisitiza kwamba lengo lao kuu ni kuishinda timu hiyo inayoongozwa na Mreno huyo mwiba kwa walinda lango.

"Unapomzungumzia Cristiano Ronaldo, unamzungumzia mmoja wa wachezaji bora zaidi duniani, na kwangu ni heshima kucheza naye kwenye uwanja mmoja...lakini lengo letu kesho ni kushinda mechi."


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved