logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nuru Okanga adai kukamatwa na DCI

Lakini pia itakumbukwa hii si mara ya kwanza anaburuzana na mkono wa sheria.

image
na Radio Jambo

Michezo29 November 2023 - 09:43

Muhtasari


• “Nimekamatwa na kupelekwa Ofisi za Dci Sababu bado haijulikani,” Okanga aliandika kwenye Facebook.

• Okanga amekuwa akisifika tangu matokeo ya Cheti cha Elimu ya Msingi nchini (KCPE) kutangazwa wiki jana

ndani ya studio za Radio Jambo.

Mwanasiasa chipukizi Nuru Okanga ameibua dai jipya kwamba ametiwa mbaroni na makachero wa DCI na kupelekwa katika kituo kikuu cha makachero hao.

Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Okanga aliandika kwamba ametiwa mbaroni na yuko chini ya ulinzi katika ofisi kuu za DIC.

Hata hivyo, Okanga alisema kukamatwa kwake hakuna sababu yoyote na wala mwenyewe hajapewa sababu zozote za kukamatwa.

“Nimekamatwa na kupelekwa Ofisi za Dci Sababu bado haijulikani,” Okanga aliandika kwenye Facebook.

Okanga amekuwa akisifika tangu matokeo ya Cheti cha Elimu ya Msingi nchini (KCPE) kutangazwa wiki jana.

Mwanaharakati huyo mwenye sauti kubwa anayetazama kiti cha MCA wa Kholera, kaunti ya Kakamega alikuwa miongoni mwa watahiniwa waliofanya mitihani ya kitaifa ya shule za msingi, na Wakenya wengi walikuwa wakitazamia kujua jinsi alivyofaulu.

Okanga bado hajaeleweka kuhusu utendakazi wake katika mitihani ya KCPE, na kuwafanya baadhi ya watumiaji wa mtandao kuhitimisha kuwa huenda alijiandikisha kwa karatasi chache kuliko alivyowafanya waamini.

Mwishoni mwa wiki jana katika mahojiano kwenye stesheni ya Radio Jambo, licha ya juhudi zote za kubembelezwa, Okanga alikataa kata kata kuweka wazi alama alizozipata kwenye KCPE.

Lakini pia itakumbukwa hii si mara ya kwanza anaburuzana na mkono wa sheria.

Mtetezi huyo wa sera za ODM na Raila Odinga amekuwa akimenyana na serikali kwa kuikosoa akitumia maneno makali tena bila woga, jambo ambalo limemfanya kuwa mgeni wa makachero kila mara.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved