logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Erik ten Hag afichua kuonywa dhidi ya kukubali kibarua cha kuifunza Man Utd

“Walisema haiwezekani. Mimi? Nilitaka changamoto.," alisema.

image
na Davis Ojiambo

Michezo11 December 2023 - 07:45

Muhtasari


  • • Ten Hag alimaliza kipindi cha miaka sita cha kusubiri kwa klabu kupata taji la fedha kwa kunyanyua Kombe la Carabao mwezi Februari.
Erik ten Hag

Kocha wa Manchester United, Erik ten Hag amefichua kuwa alionywa asiwe meneja wa Manchester United kwa sababu ilionekana kuwa kazi "isiyowezekana".

Mholanzi huyo mwenye umri wa miaka 53 alihamia Old Trafford kutoka Ajax mnamo 2022 lakini amepata shinikizo katika msimu wake wa pili katika nafasi hiyo.

United wanashika nafasi ya sita kwenye jedwali la Ligi ya Premia kufuatia ushindi wa mabao 2-1 Jumatano jioni dhidi ya Chelsea, pointi tisa nyuma ya vinara Arsenal, huku wakiwa wametatizika barani Ulaya.

"Kila mtu alikuwa akiniambia, 'huwezi kufanikiwa katika kazi hiyo'," Ten Hag aliambia mashabiki wa United We Stand.

“Walisema haiwezekani. Mimi? Nilitaka changamoto. Nilijua haingekuwa rahisi, lakini ilikuwa klabu kubwa yenye mashabiki wengi. Watu wanaipenda Manchester United, au wako dhidi ya Manchester United. Napenda vilabu kama hivi. Ajax ilikuwa hivi."

Ten Hag alimaliza kipindi cha miaka sita cha kusubiri kwa klabu kupata taji la fedha kwa kunyanyua Kombe la Carabao mwezi Februari kabla ya kumaliza ligi katika nafasi ya tatu.

Hata hivyo, kikosi chake hakiko kwenye kasi msimu huu kufuatia vipigo sita kutoka kwa mechi 15 za ligi, pamoja na kukaa mkiani mwa kundi lao la Ligi ya Mabingwa huku ikiwa imesalia na mechi moja - nyumbani dhidi ya Bayern Munich wiki ijayo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved