logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Messi huenda akakosa mechi dhidi ya Ecuador kufuatia jeraha

Messi, ambaye aliumiza misuli ya paja la kulia dhidi ya Chile, hakucheza mechi ya fainali ya kundi dhidi ya Peru.

image
na Davis Ojiambo

Michezo04 July 2024 - 07:33

Muhtasari


  • •Messi, ambaye aliumiza misuli ya paja la kulia dhidi ya Chile, hakucheza mechi ya fainali ya kundi dhidi ya Peru.
  • •“Tutajaribu iwezekanavyo ili acheze na iwapo hawezi, tutatafuta suluhisho jingine kwa timu,' alisema Scaloni
Lionel Messi

Kocha wa Argentina, Lionel Scaloni, amesema kuwa bado anashuku iwapo nahodha wa timu yake, Lionel Messi, atacheza kwenye mechi ya robo fainali dhidi ya Ecuador mnamo Alhamisi kwenye uga wa NRG kufuatia kuumia kwenye misuli ya paja.

Messi, ambaye aliumiza misuli ya paja la kulia dhidi ya Chile, hakucheza mechi ya fainali ya kundi dhidi ya Peru. Kocha Scaloni, vilevile, alikosa mechi hiyo kufuatia kupata marufuku ya kutohudhuria mechi moja na CONMEBOL.

CHIO“Tutangoja masaa machache ndipo tufanye uamuzi. Siku nyingine huwa bora. Tutaamua kulingana na ujumbe tutakaopata leo,” Scaloni aliambia vyombo vya habari baada ya Messi kuonekana akiwa mazoezini na timu.

“Tutajaribu iwezekanavyo ili acheze na iwapo hawezi, tutatafuta suluhisho jingine kwa timu. Naenda kuzungumza naye leo na nadhani itakuwa bora achukue muda wake afanye mazoezi kadri awezavyo.”

Mabingwa watetezi Argentina wanatumai kushinda taji lao la 16 la Copa America. Watamenyana na timu ya umahiri, Ecuador, ambao walinyakua nafasi yao kwenye robo fainali baada ya kumaliza nafasi ya pili kwenye kundi B. Ecuador walinyakua nafasi hiyo baada ya kutoka sare ya 0-0 na Mexico.

“Ecuador ni kikosi kizuri kwa kuwa wana wachezaji bora na kocha bora. Ni miongoni mwa timu bora kwenye Copa America. Wana nafasi nzuri ya kuwania kwenye ubingwa wa taji,” Scaloni alisema.

Mbali na hayo, Scaloni aliongezea kuwa maonyesho hayo ya bara yalikuwa yamethibitisha kuwa mashindano bora ya kiwango cha juu kwani hamkuwa na upendeleo kwa atakayeshinda taji.

“Yeyote anaweza fika fainali kwa urahisi na kushindana na walio bora ulimwenguni. Kwenye michezo ya jana kati ya Colombia na Brazil, mchezo huo ulikuwa wa hali ya juu. Uruguay, vilevile, wanafanya vyema na si jambo la kushtua,” alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved