Kenya imepangwa katika kundi J la michuano ya kufuzu kwa Afcon 2025.
Droo ya makundi ya kufuzu kwa Afcon 2025 ilifanyika Julai 4, 2024 katika jiji la Johannesburg, Afrika Kusini wakati makundi kumi na mawili yenye timu nne kila moja yalipoundwa.
Katika kundi J, Kenya inashiriki pamoja na Cameroon, Namibia na Zimbabwe.
Mechi za makundi zitaanza mwezi Septemba 2024 na kumalizika Novemba 2024 kabla ya mchuano mkuu utakaoanza tarehe 21 Desemba mwaka ujao, na fainali kuchezwa tarehe 18 Januari 2026.
Miamba wa soka kutoka Afrika Kaskazini, Morroco watakuwa wenyeji wa mashindano ya mwaka ujao.
Tazama makundi mbalimbali ya kufuzu Afcon 2025:
Kundi A: Tunisia, Madagascar, Comoro, Gambia
Kundi B: Morocco, Gabon,Jamhuri ya Afrika ya Kati, Lesotho
Kundi C: Misri, Cape Verde, Mauritania, Botswana
Kundi D: Nigeria, Benin Libya, Rwanda
Kundi E: Algeria, Equatorial Guinea, Togo, Liberia
Kundi F: Ghana, Angola, Sudan, Niger
Kundi G: Cote d'Ivoire, Zambia, Sierra Leone, Chad
Kundi H: DR Congo, Guinea, Tanzania, Ethiopia
Kundi I: Mali, Msumbiji, Guinea Bissau, Eswatini
Kundi J: Cameroon, Namibia, Kenya, Zimbabwe
Kundi K: Afrika Kusini, Uganda, Kongo, Sudan Kusini
Kundi L: Senegal, Burkina Faso, Malawi, Burundi