logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Faith Kipyegon, Chebet na Wanyonyi wateuliwa kuwania tuzo ya mwanariadha bora duniani

Wanariadha hao walifanya vyema katika mashindano mbali mbali ya riadha mwaka huu

image
na Brandon Asiema

Michezo21 October 2024 - 16:01

Muhtasari


  • Tuzo hizo zinahusisha wanariadha wa kike na kiume kutoka duniani kote waliokimbia katika mashindano mbali mbali ya riadha.
  •  Emmanuel Wanyonyi ameteuliwa kwa tuzo hizo baada ya kushinda dhahabu kwenye mbio za mita 800 kwenye Olimpiki na Diamond League.

    Wanariadha kutoka Kenya wanazidi kushamiri katika majukwaa ya kimataifa baada ya baadhi yao kuteuliwa kwenye orodha ya wanaowania tuzo ya mwanariadha bora wa mwaka katika mwaka wa 2024.

    Tuzo hizo zinahusisha wanariadha wa kike na kiume kutoka duniani kote waliokimbia katika mashindano mbali mbali ya riadha.

    Tuzo hizo zinazoandaliwa na shirikisho la riadha duniani, zinalenga kutambua wanariadha waliofanya vyema katika mashindano ya Olimpiki yaliyofanyika Paris, nchini Ufaransa.

    Upande wa wanawake, Mkenya Faith Kipyegon ameteuliwa kuwania tuzo hizo baada ya kushinda mbio za mita 1,500 sawia na kuweka rekodi ya dunia katika mbio hizo.

    Vilevile kwenye tuzo hizo hizo Mkenya Beatrice Chebet ameteuliwa baada ya kushinda mbio za mita 5,000 na 10,000 pamoja na kuandikisha rekodi mpya ya dunia kwa mbio za mita 10,000.

    Upande wa wanaume, Emmanuel Wanyonyi ameteuliwa kwa tuzo hizo baada ya kushinda dhahabu kwenye mbio za mita 800 kwenye Olimpiki na Diamond League.

    Wakenya hao wanatarajia ushindani mkubwa katika kura kutoka kwa wanariadha wengine ikiwemo Julien Alfred (Saint Lucia), Sydney McLaughlin(USA), Marileidy Paulino (Dominican Republic) na Gabby Thomas (USA) kwa upande wa wanawake.

    Emmanuel Wanyonyi naye anatarajia ushindani mkubwa kutoka kwa Rai Benjamin, Grant Holloway na Noah Lyles wote wa USA pamoja na Letsile Tebogo wa Botswana.

    Mchakato wa kupiga kura utakamilika tarehe 27.



    RADIO JAMBO FREQUENCIES

    Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


    logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved