logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wanajeshi waonyeshwa kivumbi Machakos

Enock Machaka aliiweka Talanta kifua mbele kupitia bao alilopachika wavuni mnamo dakika ya 36.

image
na Tony Mballa

Michezo27 November 2024 - 19:05

Muhtasari


  •  Ulinzi, ambao walimletea mshambuliaji Enosh Ochieng katika dakika za mwisho, walikaribia kusawazisha wakati Brian Kafero alipiga mwamba wa goli zikiwa zimesalia dakika sita.
  • Kichapo hicho kilikuwa cha tatu kwa vijana wa Dunstan Nyaudo msimu huu.

Mechi ya Ligi Kuu ya Kenya kati ya Talanta na Ulinzi Stars



Klabu ya Talanta iliandikisha ushindi wa pili msimu huu baada ya kuifunga Ulinzi Stars 1-0 kwenye Uga wa Kenyatta, mjini Machakos.

Enock Machaka aliiweka Talanta kifua mbele kupitia bao alilopachika wavuni mnamo dakika ya 36.

Ulinzi, ambao walimletea mshambuliaji Enosh Ochieng katika dakika za mwisho, walikaribia kusawazisha wakati Brian Kafero alipiga mwamba wa goli zikiwa zimesalia dakika sita.

Kichapo hicho kilikuwa cha tatu kwa vijana wa Dunstan Nyaudo msimu huu.

"Nilikuwa nimeionya timu yangu kuhusu kucheza timu ambayo ilikuwa na hamu ya kupata pointi na ikaja kutuuma," Nyaudo alisema.

  “Huyu itabidi nijilaumu kwa hilo. Tulizidiwa katika safu ya kiungo na hiyo ni juu yangu kwa kutopata mbinu sawa. Nia yangu sasa iko kwenye Mathare United ijayo."

Ushindi huo uliwapeleka Talanta kukwea hadi nafasi ya 13 wakiwa na alama tisa, huku Ulinzi wakisalia nafasi ya 12 kwa alama 10.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved