Riadha

Mkenya Beatrice Chepkoech avunja rekodi ya dunia ya mbio za kilomita 5

Muda bora Zaidi ulikuwa 14:44 uliosajiliwa na raia wa New Zealand Sifan Hassan mwaka wa 2019.

Muhtasari
  • ‘ Ingawaje kulikuwa na upepo mkali  nilimudu kukimbia vizuri’ amesema
  •  Muda bora Zaidi ulikuwa 14:44 uliosajiliwa na raia wa New Zealand  Sifan Hassan mwaka wa 2019.
Beatrice Chepkoech

 Mkenya  Beatrice Chepkoech  amesajili rekodi mpya ya dunia siku ya jumapili kwa kushinda mbio za kilomita tao huko Monaco .

 Mwanariadha huyo mwenye umri wa miaka 29  aliongeza sekunde moja  kwa kusajili muda wa  dakika 14 na sekunde 43 na kujizidishia rekodi kando na ile ya mbio za mita 3000 kuruka viunzi na maji .

‘ Ingawaje kulikuwa na upepo mkali  nilimudu kukimbia vizuri’ amesema

 Muda bora Zaidi ulikuwa 14:44 uliosajiliwa na raia wa New Zealand  Sifan Hassan mwaka wa 2019.

 Mganda  Joshua Cheptegei  ndiye aliyeshinda mbio hizo kwa upande wa wanaume  kwa muda wa 13:13,  nje ya rekodi yake ya 12.51 aliokuwa ameandikisha Monaco  miezi 12 iliyopita .