logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ferdinand Omanyala apongeza serikali kwa kuwaunga mkono wanariadha

Omanyala  ndiye mwanariadha mwenye kasi zaidi barani Afrika katika mbio za mita 100.

image
na Davis Ojiambo

Michezo12 October 2023 - 15:12

Muhtasari


  • • Omanyala aliwapa motisha wanariadha wengi ambao hawajafanikiwa katika michezo yao akiwataka kutokata tamaa na kuendelea kufanya bidii kila.

 Mshikilizi wa rekodi ya Afrika wa mbio za mita 100  Ferdinand Omanyala amepongeza serikali kwa ufhadhili inaotoa kwa wanariadha.

Mwanariadha huyo aliwapa matumaini wanariadha watarajiwa ambao wana ndoto ya kujiunga na mchezo huo kutia bidii.

"Tunapata furaha kutoka kwa serikali wakati tunapofanya vyema katika mashindano yetu licha ya kukumbwa na changamoto nyingi serikali yetu inafanya michezo yetu kuwa rahisi kwa kutupa fedha za kufanikisha  mbio zetu kwa wakati ufaao",alisema.

Mwanariadha huyu pia aliwapa motisha wanariadha wengi ambao hawajafanikiwa katika michezo yao akiwataka kutokata tamaa na kuendelea kufanya bidii kila wakati ndiposa siku moja wapate kufurahia jasho lao.

Omanyala aliwataka wazazi na walezi kuwaunga mkono watoto wao katika kila wanachofanya,  ili kuanza kukuza vipawa vyao mapema ndiposa wafanikiwe kwa maisha kupitia talanta zao mbalibali.

"Maisha sio rahisi watu wanatuona kwenye Runinga  na kudhani tumefika huko kwa bahati lakini hatufiki huko kwa bahati nzuri  ila tumejitahidi sana kufika huko, na tumekuwa na dhamira, uthabiti na uvumilivu kumfikisha mtu yeyote pale", alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved