logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kocha wa timu ya Arsenal WFC ajiuzulu

Msako wa Kocha Mkuu mpya unaendelea na klabu itatoa tangazo zaidi mchakato huo utakapokamilika.

image
na SAMUEL MAINAjournalist

Football16 October 2024 - 10:56

Muhtasari


  • Katika taarifa iliyochapishwa kwenye tovuti rasmi ya klabu, Arsenal ilisema kuwa Jonas aliondoka mara moja baada ya kujiuzulu.
  • Mkurugenzi wa Michezo wa Arsenal Edu Gaspar alitoa shukrani za klabu kwa kocha huyo na kusifu kazi yake.

Siku ya Jumanne, Oktoba 15, Klabu ya Soka ya Arsenal ilitangaza kuondoka kwa kocha wa timu ya wanawake Jonas Eidvall.

Katika taarifa iliyochapishwa kwenye tovuti rasmi ya klabu, Arsenal ilisema kuwa Jonas aliondoka mara moja baada ya kujiuzulu.

"Tunaweza kuthibitisha kuwa Jonas Eidevall amejiuzulu wadhifa wake kama kocha mkuu wa kikosi cha kwanza cha wanawake na kutuacha mara moja," Arsenal ilisema.

Klabu hiyo yenye maskani yake jijini London ilitangaza zaidi kwamba Kocha Msaidizi wa kikosi cha kwanza cha wanawake Renée Slegers ataisimamia timu kama Kocha Mkuu wa Muda.

Huku akizungumzia hatua hiyo, Mkurugenzi wa Michezo wa Arsenal Edu Gaspar alitoa shukrani za klabu kwa kocha huyo na kusifu kazi yake.

"Tunamshukuru Jonas kwa kujitolea kwake kwa klabu na mafanikio yake hapa tangu ajiunge nasi mwaka wa 2021. Tunaheshimu sana kujitolea ambako alionyesha kwa kikosi cha kwanza cha wanawake na kutambua jukumu ambalo amecheza katika ukuaji na maendeleo ya timu ya wanawake ya Arsenal. Sote tunamtakia kila la kheri kwa siku zijazo,” Edu alisema.

"Lengo letu sasa litageukia mchakato wa kuteua Kocha Mkuu mpya, na wakati huo huo, kumuunga mkono Renée, anapochukua usukani wa timu kwa muda kuanzia na mechi mbili muhimu wiki hii," aliongeza.

Jonas alijiunga na mnamo Arsenal Juni 2021 kutoka FC Rosengard ya Uswidi, na kushinda mataji mawili ya Kombe la Ligi ya Wanawake ya Continental Tyres League katika misimu mitatu kamili akiwa Arsenal.

 Pia alisaidia timu hiyo kufika nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa ya Wanawake ya UEFA - mwaka wa 2022/23 - kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka kumi.

Wanabunduki pia wametangaza kuwa msako wa Kocha Mkuu mpya unaendelea na klabu itatoa tangazo zaidi mchakato huo utakapokamilika.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved