Eto’o ambaye sasa ni Rais wa Shirikisho la
Soka la Cameroon (FECAFOOT) alikuwa mjini humo kwa mhadhara wa Kundi la Ecobank
alipokutana na rafiki yake wa zamani, mwanamume ambaye aliwahi kucheza naye
kandanda.
Katika video ya kihisia iliyosambazwa kwenye
mitandao ya kijamii, Eto’o alionekana akiwa amezungukwa na mashabiki na wengine
waliohudhuria na alikuwa akitoka nje ya ukumbi huo wakati mtu ambaye hakuwa
amenaswa kwenye kamera alipoita jina lake.
Mwanzoni, gwiji huyo wa soka wa Cameroon
alitazama nyuma kwa muda mfupi kabla ya kuendelea, lakini kisha akasimama,
akageuka tena, na kugundua kuwa ni rafiki wa zamani.
Mwanamume huyo ambaye alivalia sare za
mlinzi aliingia kwenye fremu ya camera na uso wa Eto’o ukang’aa baada ya kumtambua.
Nyota huyo wa zamani wa Barcelona alionekana
akimsalimia rafikiye kwa uchangamfu na mchezaji huyo mwenzake wa zamani,
akamkumbatia kwa muda mfupi, na wakazungumza kwa raha kwa lugha ya Bassa’a,
lahaja ya Kikameruni.
Eto’o alionekana kuguswa sana na mara kwa
mara akaupapasa mkono wa rafiki yake walipokuwa wakikumbushana.
Wawili hao walikuwa na mazungumzo ya maana,
wakikumbuka uzoefu wao wa awali katika uwanja.
Akigeukia umati uliokusanyika karibu nao,
Eto’o alimtambulisha mtu huyo, akisema, “Alikuwa mchezaji mwenzangu. Nilicheza
naye.”
Kipindi hicho cha kugusa hisia kimevutia
watu wengi kwenye mitandao ya kijamii, huku watumiaji wengi wakimsifu Eto’o kwa
unyenyekevu wake.
Eto’o aliguswa sana na tukio hilo na
akamwelekeza msaidizi wake kuweka miadi rasmi na rafiki yake wa zamani ili
waungane tena.
Eto’o, mmoja wa wanasoka wakubwa barani
Afrika, alikuwa na taaluma kubwa, akishinda mataji manne ya Mchezaji Bora wa
Mwaka wa Afrika na kuchezea vilabu maarufu vya Uropa kama vile Barcelona,
Inter Milan na Chelsea.
Alipata mataji matatu ya kihistoria akiwa
na Inter Milan mwaka 2010 na kushinda Ligi ya Mabingwa akiwa na Barcelona.
Tangu alipostaafu mwaka wa 2019, Eto’o
ameendelea kuwa na ushawishi mkubwa katika ulimwengu wa soka, na Desemba 2021,
alichaguliwa kuwa Rais wa FECAFOOT, akiendelea kujitolea kuendeleza mchezo huo
nchini Cameroon.