Ubaguzi wa rangi

Marcus Rashford apokea matusi ya ubaguzi wa rangi mtandaoni

Shirikisho la soka la FA limeelezea kujitolea kwake katika kupambana na wanaoendeleza ubaguzi wa rangi

Muhtasari
  • "  Mimi ni mwanamme mweusi na kila siku nina fahari ya kujiita hivyo’ amesema katika twitter
  •   Nyota huyo mwenye umri wa miaka 22 aliyepewa tuzo ya MBE kwa kazi yake kupambana na  umaskini wa chakula miongoni ma watoto ,alipokea jumbe za kumbagua rangi yake jumamosi usiku baada ya kilabu yake kutoka sare tasa na Arsenal

 

Arsenal ilitoka sare tasa na Man united jumamosi
Image: Getty

 Mshambuliaji wa Manchester United Marcus Rashford  amesema amepitia ‘ukatili mkubwa Zaidi wa kibinadamu’ baada ya kutukunawa kwa msingi wa rangi yake katika mitandao ya kijamii siku ya jumaksi usiku .

  Nyota huyo mwenye umri wa miaka 22 aliyepewa tuzo ya MBE kwa kazi yake kupambana na  umaskini wa chakula miongoni ma watoto ,alipokea jumbe za kumbagua rangi yake jumamosi usiku baada ya kilabu yake kutoka sare tasa na Arsenal

"  Mimi ni mwanamme mweusi na kila siku nina fahari ya kujiita hivyo’ amesema katika twitter

 

" Hakuna yeyote ,au tamko lolote litakalonifanya nijihisi kivingine . kwa hiyo pole sana iwapo ulifikiri kwamba jibu langu litakuwa na machungu , hutalipata jibu kama hilo hapa’ ameongeza Rashford .

 Akizungumza katika kipindi cha  Match of the Day,  aliyekuwa mshambuliaji wa Arsenal na  England Ian Wright amesema maamlaka na kampuni za mitandao ya kijamii zinafaa kuchukua hatua Zaidi kukabiliana  na wanaoendeleza ubaguzi kama huo mitandaoni

 Aliyekuwa  kiungo wa kati wa   Tottenham, Newcastle  na  England  Jermaine Jenas aliongeza :  "kumbi hizi ,nazihitaji zinionyeshe watu hawa na kutoa hakikisho kwamba hatua  zinachukuliwa ili kupata  haki ,kwa wale ambao wanauliza mbona bado tunapiga goti ,jibu ndilo hilo’

 Shirikisho la soka  la FA  limeelezea kujitolea kwake katika kupambana na wanaoendeleza ubaguzi wa rangi