Everton yasimamisha kazi mchezaji mmoja kupatia nafasi uchunguzi wa polisi

Klabu hiyo ilitangaza kuwa wataendelea kushirikiana na maafisa wa usalama katika uchunguzi wao.

Muhtasari

•Klabu ya Everton nchini Uingereza imemsimamisha kazi mchezaji mmoja wa kikosi cha kwanza  ili kupatia nafasi uchunguzi wa polisi kuhusiana na tuhuma dhidi yake kuendelea.

•Hata hivyo hawakutaja mchezaji mhusika wala kesi inayomkabili

Image: GOAL

Klabu ya Everton nchini Uingereza imemsimamisha kazi mchezaji mmoja wa  kikosi cha kwanza  ili kupatia nafasi uchunguzi wa polisi kuhusiana na tuhuma dhidi yake kuendelea.

Kupitia tovuti yake rasmi, klabu hiyo ilitangaza kuwa wataendelea kushirikiana na maafisa wa usalama katika uchunguzi wao.

Hata hivyo hawakutaja mchezaji mhusika wala kesi inayomkabili. 

"Klabu itaendelea kusaidia maafisa wa usalama katika uchunguzi wao na hakuna ujumbe mwingine utatolewa kwa sasa" Everton iliandika.

Wiki chache zilizopita klabu hiyo ilimteua aliyekuwa kocha wa Liverpool  Rafa Benitez kama kocha mkuu baada ya kuondoka kwa  Carlo Ancelloti kuelekea Real Madrid  mapema mwezi huo.

Everton ilimaliza katika nafasi ya kumi msimu uliopita na kuzoa alama 59.